Sunday 28 July 2013

MSHIRIKI WA BIG BROTHER AFRICA KUTOKA TANZANIA "NANDO" AONDOLEWA KATIKA MASHINDANO (DISQUALIFIED)

Mshiriki katika shindano la big brother Africa kutoka Tanzania "Nando" ameondolewa rasmi katika mashindano hayo kwa madai ya kukiuka masharti ya shindano hilo.... Nando ambaye juzi alikorofishana na Elikem na kutupiana maneno makali ambayo yalifanya ahesabiwe kosa la pili baada ya lile la kwanza la kukutwa na kisu katika party ya Channel O na mbaya zaidi alipomtamkia Elikem kwamba "I feel like stabbing him,, these are n*ggas that deserve to die" Nando pia amekutwa na kosa lingine la tatu ambalo inadaiwa alitunza mkasi chini ya godoro anapolala n ambayo ni kinyume na sheria ya mashindano hayo,, ndipo Biggie alipotamka kwamba Nando ameondolewa katika mashindano.. Elikem nae ahesabiwa kosa la kwanza
Nando

karibu nyumbani kaka......
 Mshiriki kutoka Ethopia ambaye ni Mshkaji wa Karibu wa Nando "BIMP" ahuznika zaidi ya washiriki wote baada ya kupokea hizo habari.. ambapo Biggie Alimwita kama THE HEAD OF HOUSE lakini alionekana kupuuza maneno ya Biggie na kuendelea kulala, ndipo baadae alienda na kuambaiwa apaki nguo za mshkaji wake.
Bimp's heartache
Bimp katika mawazo mazito baada ya mshikaji wake kusepa

0 comments :

Post a Comment