Friday 18 October 2013

MAAJABU: THE ROCK NI MGAHAWA ULIOJENGWA JUU YA MWAMBA BAHARINI HUKO VISIWANI ZANZIBAR



Duniani kuna maajabu mengi,kati ya maajabu hayo ni huu mgahawa uitwao Rock uliopo visiwani Zanzibar uliojengwa juu ya mwamba mkubwa katika bahari ya Hindi..
Tazama picha zaidi hapa chini...


Mgahawa huo ulifunguliwa rasmi mwaka jana na kuna viti 45 ambapo wateja huchukuliwa na boti maalum kutoka pwani hadi kupata huduma katika mgahawa huo ili wasikanyage maji wakati wakiingia kwenye mgahawa huo.

Chakula kinachopatikana muda wote katika mgahawa huo ni samaki pekee kutoka baharini na vinywaji.
 

Wafanyakazi wa The Rock
 

The Rock umetajwa kuwa ni mgahawa wa ajabu katika Afrika Mashariki na watu wengi wakiwemo watalii hupenda kwenda kutokana na habari zake kuenenea kwa kasi na wengi hupendelea kupata hewa safi ya baharini na kuona jinsi kilivyokuwa ndani.
 

Rock, ambayo ilifunguliwa mwaka jana, inaweza kufikiwa kwa miguu, lakini pia kuna usafiri wa mashua wa kuwasafirisha wateja kutoka pwani hadi kwenye mgahawa huo.
 
teentz.com
 


 


 

0 comments :

Post a Comment