Monday 21 July 2014

HII NDIO RIPOTI MPYA KUHUSU MOHAMED SALAH KURUDI KWAO KUITUMIKIA JESHI...


Ripoti wiki hii zilionyesha kua mchezaji wa chelsea "Mohamed Salah" (22) kuhusishwa na kurudi kwao misri kuitumikia jeshi
nchini humo baada ya masomo yake kusitishwa ikiwa na maana kua alikua haruhusiwi kusafiri nje ya nchi.
Ripoti mpya zimeonyesha kua mshambuliaji huyo wa chelsea hatotakiwa kurudi kuitumikia jeshi baada ya waziri mkuu wa nchi hiyo bw.Ibrahim mahlab kuingilia swala hilo na kuitisha mkutano na viongozi wa elimu ya juu pamoja na kocha mkuu wa timu ya taifa (mpira wa miguu)  Bw. Shawky Gharib ili kujadili swala hilo...
Bw.Ibrahim alidai kua kufanya hivyo ni kuua mpira wa miguu nchini humo..
Salah sasa hatorejea kwao na ataendelea kuitumikia timu yake ya Chelsea

0 comments :

Post a Comment