Sunday 27 October 2013

HUZUNI: BABA MZAZI WA WEMA SEPETU AFARIKI DUNIA..



Taarifa zilizotufikia hivi punde zinaeleza kuwa baba mzazi wa Miss Tanzania 2006, Wema .A. Sepetu , “Balozi Isaac Abrahamu Sepetu” amefariki dunia.. Marehemu
Amefariki jijini Dar-es-salaam na Mipango ya mazishi inafanyikia nyumbani kwa marehemu maeneo ya Sinza-Mori jijini Dar. 
Habari zinaeleza kuwa Mzee Isaac Sepetu alikuwa mgonjwa kwa muda wa miezi kadha hivi karibuni na amekuwa akisumbuliwa na maradhi ya kiharusi na kisukari.
PLANET CHOICE inaitakia pole familia nzima ya Sepetu na Uvumilivu katika wakati mgumu kama huu..Mungu ailaze Roho ya Marehemu mahali pema peponi…

0 comments :

Post a Comment