Saturday 10 August 2013

LAMPARD, MATA NA LUIZ HUENDA WAKAMISS MECHI ZA UFUNGUZI WA LIGI KUU

Wachezaji machachari na tegemezi katika timu ya chelsea " Lampard, Mata na Luiz"huenda wakamiss mechi za mwanzo wa msimu wa ligi kuu ya England, hayo yamesemwa na kocha mkuu wa Timu hiyo ya Bluez.. Jose Mourinho amedai ya kwamba Lampard atakosa mechi hiyo kutokana na kuitwa katika kikosi cha timu ya taifa ya england itakayochuana na scottland jumatano ijayo.. mourinho amedai ya kua mbali na mchezaji huyo kuitwa katika timu yake ya Taifa ila bado anahitaji kufanya mazoezi kutokana na kuwa na mda chache wa mazoezi kipindi cha pre-season kwasababu ya  majeruhi
Lampard, Mata and Luiz could miss Chelsea's season opener, says Mourinho
Pia kwa upande mwingine Mourinho amedai ya kua Mata na Luiz pia watakosa mechi za ufunguzi wa msimu kutokana na kua majeruhi..Mourinho alisema kua Mata na Luiz ni wachezaji muhimu kwenye Timu na kukosekana kwao pia sio tatizo.
Barcelona walituma maombi ya kumsajili kiungo huyo wa Brazil (David Luiz) kwa euro millioni 25 lakini ofa hiyo ilikataliwa na mourinho na kusema kua hakuna mchezaji atakayeuzwa. Mourinho alisisitiza ya kwamba kama David Luiz atakosekana katika mechi hiyo ya ufunguzi ni kwasababu tu ya majeruhi.

0 comments :

Post a Comment