Saturday 15 March 2014

PICHA: HIVI NDIVYO ROSE NDAUKA NA MASTAA WENGINE WALIVYOJITOLEA KUSAFISHA JIJI..

 

Hii ni kampeni ya Rose Ndauka ambayo kaipa jina la Ng’arisha Tanzania inayohamasisha kuweka jiji la Dar es salaam katika hali ya usafi na kupendeza ambapo kampeni hii inahusisha kufagia baadhi ya mitaa katika manispaa ILALA  ili kuzoa taka na kuzitupa maeneo husika.


Kampeni ilianza majira ya saa moja asubuhi na kumalizika saa 3 asubuhi baada ya hapo ukafanyika uzinduzi wa jiko la kuchomea taka mtaa wa Lumumba katika Manispaa ya Ilala ikiwa ni kama ishara ya kuhamasisha raia wote Kuamka na Kubadilika na kuonyesha mapenzi kwa kuweka miji katika hali safi kwa kusafisha maeneo wanayoishi.

Hizi ni baadhi ya picha za mastar mbalimbali wa Tanzania walivyojumuika na Rose Ndauka katika kampeni hii.

0 comments :

Post a Comment