Thursday 5 December 2013

BREAKING NEWS: MZEE NELSON MANDELA AMEFARIKI DUNIA..



 
Habari kuhusu kifo cha Nelson Mandela zimetangazwa na Rais wa sasa wa Africa Kusini Bwana Jacob Zuma dakika chache kuelekea saa saba usiku wa kuamkia leo December 6 2013. Pia vyombo vya habari Bbc Na CNN vimetangaza kuwa Mandela amefariki akiwa na miaka 95 na alikuwa hospitalini kwa muda mrefu akipata matibabu..Endelea hapa...

CNN Wana Repoti kuwa Mwezi wa tatu mwaka 2013 Mandela aliumwa sana na raia wangi Africa Kusini walijua watampoteza Mandela ila haikuwa hivyo na hali yake ikawa nzuri kwa muda na baadae kurudishwa hospitalini baada ya kuzidiwa.

Bendera zote Africa Kusini zimeanza kupepea nusu mlingoti baada ya kutangazwa kwa kifo cha Nelson Mandela. Pia patakuwa na siku kumi za maombolezo.

Kwenye Miaka Tofauti Kazi Za Sanaa Kuhusu Maisha Ya Mandela Zimeigizwa Na Waigizaji Wakubwa Kama Sidney Poitier, Morgan Freeman, Dennis Haysbert, Danny Glover and Idris Elba.

"Ngiyabonga Tata Madiba. Thank you for sharing your life with us. Hamba Kahle Tata! May your soul rest in Eternal Peace" Ameandika Mwamvita Makaba

0 comments :

Post a Comment