Monday 28 July 2014

HUSSEIN MACHOZI ASHINDWA KUFUNGUKA ISHU YA KUFUKUZWA KENYA KWA TUHUMA ZA KUFUMANIWA NA MKE WA MTU

Mitandao mbalimbali ya nchini Kenya weekend hii zimeandika stori ya kusikitisha kuhusiana na msanii wa Bongo Flava anayeishi nchini humo,Hussein Machozi
kuwa amepewa masaa 24 na mamlaka za nchini humo baada ya kufumaniwa na mke wa mwanasiasa maarufu mjini Mombasa Moja kati ya vichwa vya habari vya story hii kinasomeka kama ifuatavyo
“msanii hussein machozi apokea kichapo cha mbwa na kupewa masaa 24 kuondoka hapa nchini kenya”. “msanii huyu mashuhuri wa bongo flavor leo hii katika hoteli flani ya kitalii hapa jijini mombasa alijipata matatani baada ya kupatikana akiwa na mke wa kiongozi flani mashuhuri wa hapa nchini. yasemekana mheshimiwa huyu amekua akimkulia timing machozi bila mafanikio lakini leo siku arobaini
zilitimia kwake msanii huyu mkosa adabu,”
Hata hivyo clouds fm ikampigia simu Hussen Machozi mwenyewe bahati mbaya
alishindwa kuzungumza lolote kuhusu ishu hii, pia hakuweza kufunguka kama yuko Kenya ama Tanzania.

Credits: Clouds Radio

0 comments :

Post a Comment