Tuesday 22 July 2014

ALIKIBA: MIMI SHABIKI WA NYIMBO ZA DIAMOND ; AELEZEA PIA CHANZO CHA BIFU YAO...

Miongoni mwa vitu vilivyokuwa vikisubiriwa kwa hamu na mashabiki wa bongo fleva wiki hii ni pamoja na kusikia
kauli ya Alikiba kuhusu chanzo cha beef kati yake na msanii mwenzake Diamond Platnumz.
Kupitia kipindi cha Sporah kilichoruka July 22 Clouds TV, Alikiba amefunguka mambo mengi ikiwemo jinsi walivyofahamiana kwa mara ya kwanza, chanzo cha beef yao na wakoje hivi sasa. Kabla hujafahamu undani wa alichokizungumza, hizi ni facts chache alizozitoa Alikiba katika Interview hiyo.
1.Alikiba ndiye alimpa ruhusa Bob Junior amrekodie
Diamond nyimbo zilizomtoa kama ‘Kamwambie’ katika
studio yao ya Sharobaro!
2.Alikiba alishirikishwa katika wimbo wa Diamond ‘Lala
Salama’!
3. Alikiba ni shabiki wa nyimbo za Diamond hadi sasa!
4. Diamond aliomba ashirikishwe katika hit ya Alikiba
‘Single Boy’!
5. Alikiba ana watoto watatu, lakini hana uhusiano tena na mama zao.

Asilimia kubwa ya kipindi ilihusu uhusiano wa Alikiba na Diamond, na hii ni sehemu ya maelezo ya Kiba.
Alikiba aliizungumzia sababu iliyozaa beef kati yake na Diamond, swali la Sporah lilikuwa kama Alikiba ana namba ya simu ya Diamond:
“Nilikuwa nayo kipindi Fulani, nilipohisi amenikosea nikaona sina ulazima…kuna kipindi alinikosea kwasababu
nilisikia amesema kwamba tulirekodi wote ile nyimbo ya ‘Single Boy’, na si kweli. Halafu anasema mimi ndio nilimfuta…
kwa kunikosea kwa Diamond nilihakikisha kutokana na mimi mwenyewe ndo nilifanya nyimbo yake ‘Lala
Salama’ iko kwenye album yake, akanifuta nikahisi amenikosea sana nilichoimba mimi akawa ameimba yeye, alichonituma nifanye nimefanya kwa mapenzi yote, na
mimi namsupport kila msanii wa Tanzania anayefanya vizuri anayeimba vizuri, sikatai anaimba vizuri sijui ukisema ame copy am proud, mi sijamaind wala nini
lakini usiseme kwa watu ukadanganya ukaonekana mi sifai, siko hivyo mimi.” Aliendelea,
“Watu wengine ambao hawaelewi vizuri wanaweza wakamwamini Diamond, kila mtu ana mapenzi yake labda kuna wengine wanampenda Diamond wengine wanampenda Alikiba. wanaweza wakawa wengine,wanampenda..Diamond wakaamini mimi nimemfuta Diamond kwenye nyimbo ya ‘Single boy’ lakini mimi
wala, shahidi producer Manecky ndo alitengeneza ile nyimbo. Sikuwahi kwenda na Diamond kwenye studio na sikuwahi kufikiria kufanya nyimbo nae.Ila alinipigia simu baada ya ile nyimbo kuleak, imevuja
Single boy, tayari nimeshafanya na Jaydee, akaisikia kwenye simu Ali kuna nyimbo nimeisikia unaonaje ile tukifanya ile itakuwa safi sana afu akanipa mpaka
idea ya video na nini, nikamwambia sawa inawezekana lakini mimi nadhani itapendeza zaidi tukifanya nyimbo
nyingine mimi na wewe,kwasababu hii tukifanya mimi na wewe haita make sense inapendeza ikiwa single boy single girl, hicho ndo kitu nilimjibu.
Akaniambia poa lakini we fikiria hiyo, nikamwambia
okay lakini hata kama nikifikiria mi sioni jibu hapo, jibu ni hilo hilo. Hicho ndo kitu ambacho nilimjibu Diamond.
Baada ya kama wiki moja nikaja kusikia kwenye mablog, mpaka nikapigiwa simu kwamba mimi nimemfuta kwenye
ile nyimbo wakati yeye ndio aliyenifuta katika nyimbo yake, shahidi producer wangu mimi KGT anaitwa
ambaye nimetoka naye muda mrefu sana..nyimbo zang zote alikuwa akiproduce yeye”. Kuhusu nani aliyemuita mwenzake kwaajili ya wimbo ambao Alikiba anadai Diamond alimfuta (Lala Salama)
“Hakuna aliyemuita mwenzake, ila mimi pale studio ambayo alikwenda kurekodi Diamond ni studi ya kwangu mimi ambayo ilikuwa imenitoa pale G-Records
na watu wote wanajua nimetokea pale. ..Nakwenda kutembea kama nyumbani , kuwatembelea stud kumtembelea producer wangu, nikamkuta Diamond nae studio anarecord. Kuingia pale ndani ya studio nikakut amesha record kabisa…akaniambia hebu sikiliza hii, nikasikiliza nikamwambia umeimba vizuri sana…
nikajaribu kumwambia ungeimba hivi na hivi na hivi ingekuwa vizuri sana ila niliheshimu mamuzi yake
kwasababu kila mtu na style yake, nikawa natak kuondoka akaniita, akaniambia nakuomba uingize zile sauti zako za juu, kila mtu anajua ukisema hivyo, kuna
sauti zangu flani hizo silaha zangu naweza kusema wengi wanapenda.
Nikamwambia nikiingiza vile nitaharibu mi nahisi umeimba vizuri sana, akaniambia imba bwana, atleast chochote kile, ndio nikaimba sasa mimi pale baada ya
kufanyaje, nimeona aibu kumkatalia mbele ya producer wangu. Ni Kwa mapenzi yote nilifanya, nikamfanyia
vizuri, kweli nilikwenda na feeling nzuri sana kwasababu nyimbo ilikuwa ndio style yangu vile vile. Lakini sasa, kwasababu hata producer wangu hakuniambia nikaja kuisikia nyimbo imetoka ameingiza
yeye vile nilivyokuwa nikiimba mimi yaani njia nilizokuwa nimepita akaingiza yeye, kwahiyo nikahisi kama amenifanya mtoto wakati mimi ni mkubwa wake na
anajua hilo”.
Baada ya Alikiba kugundua hilo alichukua hatua gani za kumuuliza Diamond au producer?
“Niligundua kabisa producer wangu kunipigia simu mimi
ilikuwa sio sawa kwasababu ile nyimbo sio yake halafu nilimpa tu uhuru wa kufanya kazi na kila msanii na nilijisikia vizuri Diamond amekuja mpaka pale studio
kwetu kufanya kazi ..
Mi nilichukua simu yangu nikampigia Diamond, alichonijibu akasema yeye mwenyewe hajui , basi mi nikaachana na haya mambo, from then nikaona hamna
tatizo lakini kwa kujua yeye alinifuta katika nyimboyake”.

Alikiba na Diamond walivyofahamiana:
“Unajua mimi Diamond nimemjua muda mrefu sana, mimi ndio nimemrelease pale akafanya nyimbo Sharobaro wakati mimi niko kwenye tour America, nilikuwa pale kama president, vice wangu alikuwa Bob
Junior ambaye ndio producer pale, akanipigia simu kwasababu hakuwa na maamuzi ya kumruhusu arekodi,
bana kuna msanii anaitwa Diamond anaimba vizuri tu, nikamwambia kama anaimba vizuri mrekodie”.
Alikaba amekiri kuwa ni shabiki wa nyimbo za Diamond lakini si shabiki wake:
“Mimi sijutii, vile vile am happy kwa yeye kufaniki kufanya kazi nzuri, amerepresent nchi yetu anajitahidi kwasababu honestly naweza kusema ukweli mimi pia
sometimes nakuwa shabiki wa music..mimi sio shabiki wa Diamond. Unapoongelea shabiki unaweza kushabikia nyimbo basi, kuna nyimbo ambazo amenifurahisha
Diamond ameimba nikasema yes amefanya vizuri, lakini sio kwamba namshabikia yeye, mi napenda music,
sikufichi mi naskiliza music ya kila msanii anayeimba vizuri, siwakubali wasanii napenda kazi zao”.
Kuhusu alivyojipanga kurudi kwenye game na kukabiliana na Diamond ambaye kwa sasa ndie msanii aliye juu zaidi:
“Kizuri kikikosekana kibaya pia kinaonekana kizuri…!!”
Sporah alimuuliza kuwa haoni kwa kipindi alichokaa kimya Diamond ndio kama amechukua nafasi yake kwenye muziki:
“Hakuna mtu aliyechukua nafasi yangu, labda kama ni kiti ambacho nilikuwa nimekaa kinavumbi na nachotakiwa ni kukipangusa tu na kukaa tena, lakini
labda yeye yuko siti nyingine ila the back seat. Formula tofauti najua sasa hivi wanahitaji nini sababu muda
ambao nimepumzika nilikuwa kama mshabiki wa muziki…
lakini sikuweza kupata muziki ule kama tulikuwa tukisikia zamani Latifah…Violet ambao ule kama wimbo wa taifa.
Na nimeona wanamiss kwasababu mafans wangu kwa upendo wao kwakweli nawashukuru sana kwa mapenzi
ambayo wamenionesha uvumilivu na kunikumbusha Ali njoo we need you…and kwa respect ambayo nimewapa
nawaambia Alikiba himself anakuja tena very soon, now new material, new look, na next level kila kitu”.
Ujumbe wa Alikiba kwa mashabiki wake:
“Asabteni tena na tena (mashabiki) malalamiko yenu nimepata sana, samahani najua nimewa letdown, kama
mlivyoona wengine wamepata chance ya kushine na wakatuwakilisha kwasbabu tu Alikiba aliwaachia nafasi
hiyo…narudi tena very soon so get ready for this na mnipokee vizuri.”
Siku mbili zijazo Alikiba ataachia wimbo wake mpya unaoitwa ‘Mwana Dar es salaam’.Stay tuned!
‘mwenyekiti’ chake ndo kaishakipangusa vumbi so wengine waende chumbani wakalale? (na watuache tulale) LOL!

Credit:bongo5.com

1 comments :

Post a Comment