Thursday 22 August 2013

GWIJI WA MUZIKI WA DANSI "MUHIDIN MAALIMU NGURUMO" AMETANGAZA RASMI KUSTAAFU MUZIKI


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhnpGct2iZ_M7YCfFgf-Yo0S4t1t-A6-p6X4Fg0wWzW_ht8PiK9Ry0VkAlXOOLmP-ysABD1DM69PmRrKOetOzxxGbdXjjf-btNpiRF3V686JrIKKgR5QWbN-6257EIaS4UyZz38pe5i6Aw/s640/Fenella+WHVUM+1540.jpg
                                  Mzee Ngurumo(katikati)
Mwanamuziki mkongwe wa bendi ya Msondo Ngoma Mzee Muhidin Maalim Gurumo amestaafu
rasmi kazi ya muziki alioifanya kwa muda wa miaka 53.
     Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Mzee  Gurumo mwenye umri wa miaka 73 amesema ameamua kustaafu kazi hiyo kwa hiari yake mwenyewe kutokana na umri wake kuwa mkubwa.
“Muziki kwangu umekuwa kama asili yangu na kazi yangu lakini nimeamua kustaafu kutokana na umri wangu na nitabaki kuwa mshauri tu kwa mwanamuziki yeyote atakayetaka ushauri wangu,”alisema  Mzee Gurumo.
Pamoja na kufanya kazi ya muziki Gurumo alisema kuwa hakupata mafanikio makubwa zaidi ya kujenga nyumba anayoishi na familia yake.
 “Mimi  nimeimba kwa muda mrefu sana lakini hata baiskeli sina,”alisema Mzee Ngurumo. Hata hivyo alisema  nashukuru kuwa ana nyumba ya kuishi na familia.
Vilevile Mzee nGurumo amewaasa vijana kuwa wabunifu na kuupenda mziki wa zamani kwani ndio chimbuko la bongofleva na kuwashauri wanamuziki wa sasa kuwa wavumilivu kukaa muda mrefu kwenye bendi moja ili hata wanapoondoka mchango wao uthaminiwe.
Mzee NGurumo  ambaye ana mke na watoto wanne alisema kuwa katika maisha yake ya muziki alifanikiwa kutunga nyimbo 60,000 na anavutiwa zaidi na mwanamziki Hussein Jumbe na Hassani Lehan Bichuka na kwa wanamuziki wa kizazi kipya anavutiwa na Nassibu Abdul ’Diamond’. 

Mwanamuziki huyo mkongwe alianza kufahamika katika tasnia ya muziki wa dansi kwenye miaka ya 1960 ambapo mwaka 1964 alikuwa miongoni mwa waanzilishi wa bendi ya Nuta Jazz na Mlimani Park.
Alidumu na Mlimani Park mpaka mwaka 1985 na kuhamia Safari Sound aliyofanya nayo kazi mpaka mwaka 1990 na kujiunga na Msondo Ngoma mpaka sasa alipoamua kutangaza rasmi kustaafu kazi hiyo ya Kimuziki.

 

0 comments :

Post a Comment